
Ali Nabwa katoweka, na sote tumezeeka
Na wale walomcheka, leo damu watapika
Aibu imewafika, kwa yote yalotendeka
Na kweli itapofika, roho zao kukatika
Pasiwepo pa kushika, hata haya kutundika
Sumu yao watapika, watafute pa kuwika
Kwa urongo kupachika, leo watajizika
Ficha fichu papatika, kukataa za hakika
Allah! Allah! Rabbana, tunusuru abdika
Msiba umetufika, na hasara kuibuka
Sote waja wa Hakika, kwa urithi kujitwika
Wake Mola tamweka, Malaika kuitika!
Ameen.
Wakatabahu,
Salim H. HIMIDI/Bwanatosha,
Paris, France,
18 Februari 2007